HALMASHAURI YA JIJI LA DODOMA
TANGAZO LA MNADA WA KUKODISHA BUSTANI YA MAPUMZIKO – CHINANGALI
Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma anawatangazia wananchi wete kuwa kutakuwa na mnada wa hadhara kwaajili ya kukodisha eneo la bustani ya Mapunziko ya Chinanagali( CHinangali Recretional Park) Iliopo jirani na uwanja wa ndege wa Dodoma. Mnada utafanyika tarehe 21 Novemba 2020 katika eneo la bustani kuanzia saa tatu kamili asubuhi. Bustani hiyo ni mradi mpya na ni eneo linalovutia sana kwa mapumziko na burudani mbalimbali ikiwemo uwanja wa kisasa wa mpira wa kikapu, Uwanja wa tennis, Mpira wa Wavu, mabwawa ya kuogelea wakubwa na watoto, eneo la michezo ya watoto, jukwaa la sanaa na GYM, Pia kuna maeneo ya kuuzia vyakula na vinywaji pamoja na eneo kubwa la maegesho ya magari
Siku yamnada kila mshiriki atatakiwa
- Kujisajili kwenye rejesta
- Kulipa dhamana ya fedha taslimu Tsh 2,000,000/ ( milioni mbili) amabayo itarudishwa mara baada yam nada kwa mshiriki amabaye hatafanikiwa
- Mshindi atalipa asilimia 25 ya kodi ya pango ya kipindi cha miezi mitatu siku ya manada na kumalizia asilimia 75 kabla ya kuanza kuendesha bustan hiyo, aidha atawajibika kulipa kodi zote za serikali kwa mujibu wa sheria za nhci
Kwa melezo zaidi piga siimu nambari 0622020211
Tangazo hili limetolewa na:-
Mkurugenzi wa Halmshauri,
Halmashuri ya Jiji la Dodoma
Chanzo the Guardian 18 November 2020